Habari
Waziri Nchemba awaomba viongozi wa dini kupiga vita dawa za kulevya
Waziri wa mambo ya ndani, Mwigulu Nchemba,amewaomba viongozi wa dini nchini kupiga vita dhidi ya dawa za kulevya.
Ameyasema hayo mjini Dodoma akifungua mkutano wa kanisa la kiinjiri la kilutheri, KKKT.
“Ninyi mna nafasi kubwa ya kutusaidia dhidi ya kupiga vita madawa ya kulevya, ninyi mpo kila eneo, nyinyi hamuhongeki, nyinyi hamna fitina, kauli yenu ushuhuda wenu na mtawanyiko wenu, mna msaada sana katika kupambana na dhidi ya madawa ya kulevya,” alisema Nchemba.
“Kwa kufichua wanaofanya hivyo, wapo miongoni mwa wananchi huko tunakoishi,” aliongeza.
BY: EMMY MWAIPOPO