Habari

Waziri wa Mambo ya Ndani SA ambaye video yake ya ngono ilivuja mtandaoni ajiuzulu

Waziri wa Mambo ya Ndani nchini Afrika Kusini, Malusi Gigaba, amejiuzulu nafasi yake hiyo wiki mbili baada ya kipande cha video inayomuonesha akijichua kusambaa kwenye mitandao ya kijamii kwa mapana nchini humo.

Taarifa kutoka ofisi ya rais ilisema Bw Gigaba ni miongoni mwa viongozi waandamizi wa chama tawala African National Congress-ANC , kujivua nafasi zao kwa heshima ya nchi yake na harakati zinazomhusu.

Bwana Gigaba amevishutumu vyombo vya usalama nchini Afrika Kusini kwa kudukua simu yake na kuachilia kipande cha vido chenye urefu wa sekunde kumi na tatu , ambayo alijitetea kuwa alimrekodia mkewe.

Gigaba ana umri wa miaka arobaini na saba , miaka ya hivi karibuni amejikuta katika mkanganyo wa mambo kutokana na kutumia madaraka yake vibaya katika huduma mbalimbali na kuisaidia familia ya wafanyabiashara ya Gupta yenye utata.

Wafanya biashara hao wenye asili ya nchini India wanahusishwa sana na kashfa kadhaa za rushwa chini ya utawala wa Rais Jacob Zuma.katika kila hali ikiwa ni pamoja na Bwana Gigaba, wamekana makosa yoyote.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents