Waziri Zarif adai Marekani haina uwezo wa kuiangamiza Iran ‘Imesimama imara kwa maelfu ya miaka, maadui wake wote wakiwa wametoweka’
Waziri wa mambo ya nje wa Iran Mohammed Javad Zarif amesema kile alichokiita ”kejeli za maangamizi” za rais wa Marekani Donald Trump haziwezi kuimaliza Iran.
Kupitia mtandao wa Twitter, Zarif amesema Iran imesimama imara kwa maelfu ya miaka, wakati maadui wake wote wakiwa wametoweka.
Goaded by #B_Team, @realdonaldTrump hopes to achieve what Alexander, Genghis & other aggressors failed to do. Iranians have stood tall for millennia while aggressors all gone. #EconomicTerrorism & genocidal taunts won't "end Iran". #NeverThreatenAnIranian. Try respect—it works!
— Javad Zarif (@JZarif) May 20, 2019
.@realDonaldTrump rightly deplores "military-industrial complex" pushing U.S. to #ForeverWars
But allowing #B_Team to trash diplomacy & abet war crimes—by milking despotic butchers via massive arms sales—achieves nothing but empowering that same complex.
Time to #DrainTheSwamp?
— Javad Zarif (@JZarif) May 20, 2019
Kwa mujibu wa shirika la habari la DW, Haya Zarif anayasema wakati mvutano ukizidi kushamiri baina ya nchi yake na Marekani, na onyo la Trump kwamba ikiwa Iran haitaacha kuitishia Marekani, basi mwisho rasmi wa Iran utakuwa umewadia.
If Iran wants to fight, that will be the official end of Iran. Never threaten the United States again!
— Donald J. Trump (@realDonaldTrump) May 19, 2019
Mahusiano baina ya nchi hizo mbili yalizidi kuzorota mwaka jana baada ya Rais Trump kuiondoa Marekani katika makubaliano kuhusu mpango wa nyuklia wa Iran, yaliyosainiwa mwaka 2015 kati ya taifa hilo la Kiislamu na nchi zenye nguvu duniani.
Mvutano huo ulichukuwa sura mpya mwezi huu pale Marekani ilipopeleka katika eneo la Ghuba manowari na ndege za kivita chapa B-52 kujibu ilichokitaja kuwa kitisho kutoka Iran ambacho haikukifafanua.