Burudani
Wazo la Leo ya Stamina ft. Fid Q kuachiwa Ijumaa hii!!
Rapper kutoka Morogoro, Stamina, anatarajia kutoa ngoma yake mpya iitwayo Wazo la Leo Ijumaa hii. Katika ngoma hiyo Stamina amemshirikisha Fareed Kubanda aka Fid Q ambaye anasema anamchukulia kama baba yake kimuziki. Hivi karibuni Stamina aka Kabwela aliachia bonus track iitwayo Moro Moro ikiwa ni version yake ya wimbo Mwanza Mwanza wa Fid.