Michezo

Wchezaji wa Stars wa mwaka 1980 wapatiwa majina ya Mitaa

Kata ya Kigoma imetoa mitaa 25 kwaajili ya kikosi cha timu ya taifa ya Tanzania (Taifa Stars) kilichoshiriki michuano ya AFCON mwaka 1980.

Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars )

Kufuatia vikao vilivyofanyika katika kata hiyo vya kupanga majina ya mitaa imeamua kutoa mitaa hiyo kwa wachezaji na makocha wote waliyoshiriki michuano hiyo kwenye eneo la Mji Mwema.

 Kata hiyo pia imetoa jina la Prof. Abdulrahman Mohamed Babu kwa mchango wake Afrika na ukombozi wa Afrika.

Kikosi cha Taifa Stars cha mwaka 1980 hiki hapa

Athumani Mambosasa

Juma Pondamali

Taso Mutebezi

Jelah Mtagwa

Leodgar Tenga

Mohamed Kajole

Husein Ngulungu

Mtemi Ramadhan

Juma Mkambi

Omari Hussein

Mohamed Masewa

Thuweni Ally

Peter Tino

Ahmed Thabit

Charles Boniface

Salim Amiri

Adolf Richard

Zamoyoni Mogela

Martin Kikwa

George Kulagwa

Uzinduzi wa mitaa hiyo ya mashujaa unatarajiwa kufanyika siku ya Jumamosi ya kwanza ya mwezi wa tisa ambapo kutachezwa mechi kati ya timu ya Manispaa ya Lake Tanganyika SC na timu ya Bukavu Dawa ya DRC.

By Hamza fumo

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents