Michezo
Wenger aipigia chepuo Arsenal derby ya London
Kuelekea mchezo wa derby ya London Kaskazini siku ya Jumamosi meneja wa klabu ya Arsenal, Arsene Wenger amewataka mashabiki wasoka kuacha kuidharau timu yake na kuiyona ‘underdogs’ dhidi ya wapinzani wao Tottenham.
The Gunners ilimaliza nje ya nne bora katika msimamo wa ligi iliyopita ikiwa ni kwamara ya kwanza tangu Wenger aichukue timu hiyo mwaka 1996.
Wenger amekitetea kikosi chake kwa kusema kuwa kipofiti na wala siyo dhaifu kama kinavyozungumzwa kuelekea mchezo huo wa derby.
“Nafikiri Tottenham ipovizuri lakini kwaupande wetu tuko borazaidi kushinda mchezo huu na hicho ndicho kitu tunachohitaji kuwaonyesha,”amesema meneja huyo wa Arsenal, Arsene Wenger.