Burudani

Weusi waeleza kilichowapeleka Afrika Kusini na kina Vanessa, Jux, Nahreel na Aika

Wiki chache zilizopita Joh makini, G-Nako, Vanessa, Jux, Nahreel na Aika walienda Afrika Kusini kwa pamoja, na haikufahamika kwa haraka kilichowapeleka licha ya watu kuhisi wameenda kushoot video.

Joh na G-Nako

Kwasababu wakati huo ndio wimbo mpya wa Nikki Wa Pili ‘Safari’ ambao amewashirikisha hao wote waliokwenda South ulikuwa umetoka, wengine walidhani huenda wameenda kushoot video ya wimbo huo lakini tatizo likawa moja, kwenye safari hiyo alikosekana Nikki hivyo ikabaki kuwa kitendawili.

Nikki Wa Pili amezungumza na Bongo5 na kuelezea madhumuni ya safari hiyo.

“Jux kuna wimbo wake alifanya na Joh Makini alikuwa anaenda kushoot South Africa, Vanessa pia alikuwa anaenda kwaajili ya shughuli zake za kikazi, kwahiyo tukaona sisi kama weusi pia tutumie nafasi hiyo kwasababu kina Vanessa tayari kule wana pakuanzia.” Alisema Nikki Wa Pili

Joh & KO
Joh Makini na rapper K.O wa Afrika Kusini

“Kila siku tumekuwa tukitaka kujaribu kufungua milango mingine mipya tofauti […] tukaona ni vizuri tujiunganishe Joh Makini na G-Nako waende waangalie connection za media kubwa, MTV, Channel O, Trace. Joh Makini pia alikuwa anataka kufanya collabo na wasanii wa kule K.O, AKA, Khuli Chana kwahiyo aende akatafute mawasiliano na hawa watu na aangalie uwezekano ni upi.”

XO SoundCity
Matunda ya connection hizo, XO imeanza kuchezwa na kituo cha Nigeria SoundCity

“Na pia alifanikiwa kupeleka video yake MTV ya XO, SoundCity na yenyewe, Channel O pia, kwahiyo naweza nikasema kuwa Joh Makini kwenda zake kule amefanikiwa kutengeneza link na artist wa kule na industry ya kule amefanya video pia na Jux, na pia ameweza kujua nini kinahitajika na nini kinawezekana kwahiyo saizi chochote akitaka kufanya labda ni video ni collabo au kutuma nyimbo ana sehemu ya kuanzia, ni tofauti sana na mara ya kwanza tulikuwa hatuna uelewa, kwahiyo itatusaidia sisi kufanya plan zetu zingine.” Alimaliza Nikki.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents