Burudani
Weusi warekodi wimbo na rapper AKA wa Afrika Kusini
Kundi la Weusi usiku wa kuamkia leo limerekodi wimbo na rapper wa Afrika Kusini, Kiernan Jordan Forbes maarufu kama AKA.
Rapper huyo yupo nchini kwaajili ya kuhudhuria ‘Zari All-White Party’ inayofanyika Ijumaa hii Mlimani City.
Joh Makini, Nick wa Pili na G-Nako pamoja na AKA waliungana na producer Tuddy Thomas kwenye session ya usiku huku beat ya collabo hiyo ikifanywa na Nahreel.
“TOKA STUDIO NOW….ITS DONE WEUSI FT AKA….BIG S/O @diamondplatnumz…KWA KUMLETA AKA TZ..BILA WEWE HII COLABO ISINGEWEZEKANA …S/O @adamchomvu BABA LA BABA…S/O @nahreel ON THE BIT..@tuddthomas on the session,” ameandika Nick wa Pili kwenye Instagram.