Technology
WhatsApp yafikisha watumiaji bilioni moja duniani
App maarufu ya ujumbe, WhatsApp, imefikisha watumiaji bilioni moja wanayoitumia kila mwezi.
Idadi hiyo ni sawa na mtu mmoja katika kila watu saba duniani.
App hiyo inayomilikiwa na Facebook imeizidi hata Facebook Messenger yenye watumiaji milioni 800 kila mwezi. Kampuni hiyo ilisema kuwa ujumbe bilioni 42, video milioni 250 hutumwa kwenye WhatsApp kila siku.