Technology

WhatsApp yajipanga kuanzisha huduma ya kutuma na kupokea fedha

Huduma ya kutuma ujumbe kubwa zaidi duniani, WhatsApp, hivi karibuni itawaruhusu makumi kwa mamilioni ya watumiaji wake kutuma kitu muhimu zaidi ya picha ama video – fedha.

WhatsApp inailenga zaidi India, soko lake kubwa zaidi kwa uwezekano wa kuingia katika malipo ya mtandaoni. App hiyo inayomilikiwa na Facebook, inaajiri mkurugenzi wa kuongoza jitihada hizo za malipo ya dijitali katika nchi hiyo ya Kusini mwa Asia.

Huduma hiyo itashirikiana na mabenki katika kusaidia miamala ya kidijitali kwa kutumia WhatsApp. India ina watumiaji wa WhatsApp milioni 200 kila mwezi ambayo ni moja ya tano ya watumiaji wake wote hivyo si jambo la kushangaza kuona imelengwa yenyewe kwanza.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents