Afya

WHO: Janga la Corona huenda likaisha ndani ya miaka miwili

Mkuu wa Shirika la Afya Duniani (WHO) amesema kuwa anamatumaini janga la corona litakomeshwa ndani ya miaka miwili Akizungumza mjini Geneva, Tedros Adhanom Ghebreyesus alisema homa ya Spanish flu ya mwaka 1918 ilichukua miaka miwili kudhibitiwa.

Lakini ameongeza kuwa kuimarika kwa teknolojia ya sasa huenda haenda ikasaidia ulimwengu kudhibiti virusi ndani ya “muda mfupi”.

“Bila shaka watu wakiendelea kutangamana, watatoa nafasi kwa virusi kusambaa,” alisema.

“Lakini licha ya hayo, tuna teknolojia ambayo inaweza kukomesha hali hiyo, na elimu ya jinsi ya kukomesha maambukizi,” alisema, akisisitiza umuhimu wa “umoja wa kitaifa, mshikamano wa ulimwengu”.

Mafua ya mwaka 1918 yaliwaua watu karibu milioni 50 duniani.

Coronavirus kufikia sasa imewaua karibu watu 800,000 na wengine karibu milioni 23 kuambukizwa virusi vya ugonjwa huo

Dkt Tedros pia alijibu maswali kuhusu ufisadi unaohusishwa na vifaa ya kinga binafsi (PPE) wakati wa janga la corona, na kutaja ufisadi huo kama “uhalifu”.

“Ufisadi wa aina yoyote haukubaliki,” alijibu.

“Hatahivyo ufisadi unaohusisha PPE… kwangu mimi binafsi na mauaji. Kwasababu wahudumu wa afya kufanya kazi bila PPE, tuna hatarisha maisha yao. Na pia kuhatarisha maisha ya watu wanaowahudumia.”

Japo swali linaohusiana na ufisadi liliangazia zaidi Afrika Kusini, nchi kadhaa zinakabiliwa na suala hilo.

Siku ya Ijumaa, maandamano yalifanywa mjini Nairobi Kenya kufuatua madai ya ufisadi wakati wa janga la corona, huku madaktari katika hospitali kadhaa za umma wakifanya mgomo kwa kutolipwa marupurupu na kukosa vifaa kinga

A protester wears a mask which reads: "Arrest Covid millionaires"
Maandamano yalifanyika Nairobi Siku ya Ijumaa

Hali koje sehemu zingine duniani?

Siku ya Ijumaa, nchi kadhaa zilitangaza kuwa na ongezeko la juu zaidi ya maambukizi ndani ya mwezi mmoja.

Korea Kusini ilirekodi maambukizi ya 324 wapya – idadi ambayo ni ya juu zaidi ndani ya siku moja tangu mwezi Machi.

Nchi kadhaa za Ulaya pia zilishuhudia ongezeko la maabukizi.

Viwango vya maambukizi vimeongezeka mara mbili zaidi nchini Lebanon tangu kutokea kwa mlipuko mjini Beirut ambapo watu 178 waliuawa na maelfu ya wengine wengine kujeruhiwa Agosti 4.

Mkasa huo uliwaacha bila makao karibu watu 300,000 hali ambayo iliathiri sana juhudui za kukabiliana na maambukizi ya corona.

Barani Afrika viwango vya maambukizi ya kila siku vimeshuka akatika kile Mkuu wa Kituo cha Kudhibiti na Kuzuia magonjwa, Dkt John Nkengasong, dametaja kuwa “ishara ya matumaini”.

Viwango vya maambukizi ya kila siku katika bara hilo vilikuwa 10,300 hii ikilinganishwa na 11,000 wiki iliyopita.

Je Afrika inastahili kusherehekea?

Anne Soy, BBC News, Nairobi

Baada ya idadi ya wanaothibitishwa kupata maambukizi kuongezeka barani Afrika, wiki hizi ambazo zimeshuhudia kupungua kwa idadi ni faraja kubwa.

Lakini hilo linastahili kuchukuliwa kwa tahadhari kubwa.

Hivi karibuni, idadi ya wanaopimwa imekuwa ikiongezeka hadi zaidi ya milioni 10, kulingana na kituo cha CDC Afrika.

Hiyo ni karibu asilimia 1 ya idadi ya watu barani Afrika.

Hata hivyo, Afrika Kusini inaongoza kwa idadi ya wanaopimwa na wanaothibitishwa kupata maambukizi.

Shirika la Afya Duniani (WHO) limethibisha kuwa idadi ya maambukizi mapya imekuwa ikipungua nchini Afrika Kusini siku za hivi karibuni.

Lakini pia kupungua kwa idadi ya wanaopimwa, kuna maanisha kwamba vigumu kupata picha kamili ya jinsi ilivyo.

Huenda ikawa ni mapema mno kutabiri kuwa idadi ya wanaothibitishwa kupata maambukizi mapya itaendelea kupungua.

Dkt. Nkengasong pia alisema kwamba zaidi ya vipimo milioni moja vimekuwa vikifanyika kote barani humo huku Afrika Kusini ikiwa moja ya inayopima watu kwa wingi zaidi.

Idadi ya maambukizi na vifo imepungua ikilinganishwa na sehemu zingine duniani kama vile Ulaya, Amerika Kusini na Marekani ambayo pekee imerekodi visa zaidi ya 5,500,000, lakini baadhi ya wataalamu wameonya kwamba huenda kukawa na maambukizi zaidi ya vilivyorekodiwa Afrika kwasababu ya ukosefu wa vipimo.

Usambaaji wa virusi unaonekana kupungua Afrika lakini tangu mwanzo wa janga idadi ya maambukizi ilikuwa chini kisha ikaanza kuongezeka taratibu hasa Afrika Kusini.

Afrika Kusini imerekodi maambukizi 596,060 ya virusi vya corona, kulingana na data ya Chuo Kikuu cha Johns Hopkins. Hii ni zaidi ya nusu ya maambukizi Afrika na ni nchi ya tano katika orodha ya zile zenye idadi kubwa zaidi ya maambukizi duniani.

Hata hivyo idadi ya maambukizi nchini humo imekuwa ikipungua. Kilele cha ugonjwa huo, zaidi maambukizi 12,000 mapya yalikuwa yakirekodiwa kila siku, na idadi hiyo imepungua hadi wastani wa maambukizi 5,000.

Nchi ya Afrika nyengine itakayoingia kwenye orodha hiyo ni Misri, ambayo ni ya 31 katika orodha ya dunia kwa maambukizi 96,914.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents