Willian ang’ara FA Cup aisaidia Chelsea kuiadhibu Hull City
Willian hapo jana usiku aling’ara katika michuano ya FA na baada ya kutuipia mawili katika ushindi wa magoli 4 – 0 ambao timu yake ya Chelsea uliupata dhidi ya Hull City mchezo uliyopigwa dimba la Stamford Bridge.
Katika mchezo huo uliyowawezesha The Blues kusonga mbele Willian aliipatia bao dakika za mapema tu za kipindi cha kwanza huku Pedro akitupia moja na Giroud akikamilisha karamu ya mabao katika mtanange huo.
Kikosi cha Chelsea: Caballero (7), Rudiger (7), Cahill (7), Ampadu (8), Zappacosta (7), Drinkwater (7), Fabregas (8), Emerson (7), Pedro (8), Willian (9), Giroud (8).
Waliyokuwa benchi: Scott (6), Hudson-Odoi (7)
Kikosi cha Hull: Marshall (7), Clark (5), MacDonald (5), Dawson (6), Meyler (5), Irvine (6) Stewart (5), Wilson (6), Diomande (5), Evandro (5), Dicko (5).
Benchi: Toral (6), Batty (6), Campbell (6)
Mchezaji bora wa mchezo huo ni Willian