Burudani
Witness kutoka na mdogo wake
MWANAMUZIKI Witness Fred Mwaijange ‘Witness’ amesema hivi sasa anajiandaa kufanya video mpya ya wimbo wake wa Rock star ambayo anaamini itakuwa babu kubwa kutokana na kujipanga zaidi kimuziki.
mwanamuziki huyo alisema kwamba katika wimbo huo, ambao amempa shavu mdogo wake ambaye ni mkali wa nyimbo za Ki-Nigeria. alisema wimbo huo ni badala ya ule alioimba na mumewe Mussa Ayoub ‘Mokeyz’ wa Shssssssssss.
Pia alidokeza kidogo kwa kusema wimbo wa Shssss, umechelewa kwakuwa Producer & Editor alipata ajali na kufanya kusimamisha kazi kwa muda kidogo.