Burudani

Wiz Khalifa ashtakiwa kwa kuiga nyimbo “Most of Us”

Jibril Thomaz anayefahamika jukwaani kama Wiz Khalifa ambaye alizaliwa Cameron ameshtakiwa kwa ukiukaji wa hakimiliki ya ngoma yake “Most of Us” ambayo ipo kwenye albamu yake ya Khalifa 2016.

kutokana na taarifa za Billboard Rapa anayefahamika kama Cymple Man amesema kwamba Khalifa ameiga jina la wimbo wake aliouachia mwaka 2010. Katika malalamiko, Cymple Man amesema kwamba alikutana na Khalifa mwaka 2012 katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Salt Lake City uliopo Utah nchini Marekani, ambapo Cymple Man alimpa Khalifa nakala mbili za demo ya albamu yake ya kwanza na wimbo huo ukiwemo ndani yake.

Na Raheem Rajuu

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents