Burudani

Wiz Kid kuachia project mpya

Wiz Kid ndiye msanii pekee kwa sasa Afrika anayeongoza kushirikishwa na kushiriki katika ngoma kubwa za wasanii na kupelekea kupata tuzo kama BMA(Billboard Music Awards) ambapo alifanikiwa kunyakua tuzo tatu akiwa na rapper Drake.

Msanii huyo kutoka Nigeria anatarajia kuachia project yake mpya mwezi huu ifikapo tarehe 14, project hiyo inayoitwa “Sounds From The Other Side” (SFTOS) itakuwa na ngoma zipatazo kumi na mbili.

Kupitia mtando wa Instagram msanii huyo ameshare cover ya project yake hiyo itakayo kuwa na ngoma kama ‘Dirty Wine, One For Me, Gbese ngoma ambayo amemshirirkisha Trey Songz.

“Big up my fans for the continuous support and love!! Sharing our good energy with the world! Hope u Enjoy and stay happy ! #SFTOS! ❤️ July 14th,” ameandika Wiz.

Na Laila Sued

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents