Burudani

Wizkid amfanyia umafia Drake

Drake amemtibua nini Wizkid? Hilo ndio swali ambalo watu wanajiuliza kwa sasa.

Wizkid kutoka Nigeria anadaiwa kumu-unfollow rapper Drake kwenye mtandao wa Instagram. Jumapili ya jana ilikuwa ni siku ya kuzaliwa ya Wiz, lakini aliwashtua watu kutokana na ujumbe aliouandika katika mtandao huo ambao moja kwa moja ulionekana kulenga kutokana na kitendo alichomfanyia Drake.

“From today, I give no fucks..Welcome to my world,” ameandika muimbaji huyo wa Nigeria kwenye mtandao huo.

Ijumaa iliyopita WizKid aliachia Mixtape yake yenge ngoma 12 na wimbo mmoja wa bonus, huku mixtape hiyo ya ‘Sounds From The Other Side'(SFTS) imewakutanisha mastaa kadhaa wa Marekani akiwemo Drake, Trey Songz, Chris Brown, TY Dolla $ign, Major Lazer na Bucie.

Na Laila Sued

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents