Fahamu

Yadaiwa tajiri wa kwanza na wa muda wote alitoka Afrika, Ifahamu historia yake

Yadaiwa tajiri wa kwanza na wa muda wote alitoka Afrika, Ifahamu historia yake

Mwanzilishi wa Amazon Jeff Bezos ndiye mtu tajiri zaidi duniani , kulingana na orodha ya jarida la Forbes la 2019 iliotolewa wiki hii. Akiwa na mali yenye thamani ya $131bn (£99bn) ndiye mtu tajiri zaidi duniani. Lakini yeye sio mtu tajiri kuwahi kuishi duniani. Taji hilo linadaiwa kumilikiwa na Mansa Musa , mfalme wa karne 14 kutoka Afrika Magharibi ambaye utajiri wake ungeathiri uchumi wa taifa zima.

Kwa mujibu wa BBC. Akaunti zake zilikuwa na utajiri mkubwa kitu ambacho ilikuwa vigumu kuweza kubaini thamani ya utajiri na uwezo wake ,kulingana na Rudolph Butch profesa wa Historia katika chuo kikuu cha california .

Mansa Musa alikuwa tajiri zaidi ya mtu yeyote angeweza kuelezea, Jacob Davidson aliandika kuhusu mfalme huyo wa Afrika katika tovuti ya Money.com mwaka 2015.

Mwaka 2012 Tovuti ya Marekani iliweka thamani yake kuwa $400bn, lakini wanahistoria wa kiuchumi wanakubaliana kwamba mali yake haikuweza kuhesabiwa kwa kutumia nambari.

The 10 richest men of all time

Watu matajiri zaidi kuwahi kuishi duniani.

  • Mansa Musa (1280-1337, Mfalme wa Mali ambaye mali yake haiwezi kuelezewa
  • Augustus Caesar (63 BC-14 AD, Mfalme wa Roma ) $4.6tn (£3.5tn)
  • Zhao Xu (1048-1085, Mfalme wa Shenzong of Song China) mali yake haikuweza kuhesabika
  • Akbar I (1542-1605, Mfalme wa Mughal India) mali yake haikuweza kuhesabika
  • Andrew Carnegie (1835-1919, Mfanyibiashara wa viwanda wa Uscochi na Marekani ) $372bn
  • John D Rockefeller (1839-1937) Mfanyibishara wa Marekani ) $341bn
  • Nikolai Alexandrovich Romanov (1868-1918, Tsar wa Russia) $300bn
  • Mir Osman Ali Khan ( 1886-1967, Ufalme wa India ) $230bn
  • William The Conqueror (1028-1087) $229.5bn
  • Muammar Gaddafi (1942-2011, long-Mtawala wa Libya) $200bn

Chanzo: Money.com, thamnai ya watu maarufu

Mfalme wa dhahabu

Mansa Musa alizaliwa 1280 katika familia ya watawala. Nduguye , Mansa Abu-Bakr, alitawala ufamle huo hadi 1312, wakati alipoamua kwenda safari.

Kulingana na mwanahistoria wa karne ya 14 Shibab al-Umari, Abu-Bakr alipendelea sana kuiona bahari ya Atlantic na kile ilichokuwa nacho.

Aliripotiwa kuanza safari na msafara wa meli 2000 na maelfu ya wanaume na wanawake pamoja na watumwa. Walienda na hawakurudi tena.

Wengine kama vile mwanahistoria wa Marekani Ivan Van Sertima anadai kwamba waliwasili Marekani Kusini. Lakini hakuna ushahidi.

Ukweli ni kwamba Mansa Musa alirithi ufalme ulioachwa nyuma na nduguye. Chini ya uongozi wake ufalme wa Mali uliimarika kwa kiwango kikubwa.

Aliunganisha miji 24 ikiwemo Timbuktu.

Ufalme wake ulipanuka kwa takriban maili 2000 kutoka bahari ya Atlantic hadi nchini Niger akichukua sehemu ambazo ndizo Senegal ya sasa, Mauritania, Mali, Burkina Faso, Niger, The Gambia, Guinea-Bissau na Ivory Coast.

Ardhi hizo zote zilikuwa na mali asli kama vile dhahabu na chumvi.

Wakati wa Utawala wa Mansa Musa, ufalme wa Mali ulikuwa ukimiliki takriban nusu ya dhahabu zote duniani, kulingana na kumbukumbu ya Uingereza.

Na mali yote hiyo ilimilikiwa na mfalme huyo. Kama kiongozi, Mansa Musa alikua na uwezo wa kufikia utajiri wa kiwango chochote kile duniani, Kulingana na Kathleen Bickford, ambaye ni mtaalam wa sanaa ya Afrika katika chuo kikuu cha NorthWestern.

Vituo vikuu vya kibiashara ambavyo vilikuwa vikifanya biashara ya dhahabu na bidhaa nyengine vilikuwa chini ya himaya yake na alijipatia mali nyingi kupitia biashara hiyo, aliongezea.

Safari ya kuelekea Mecca

Ijapokuwa mfalme huyo wa Mali alikuwa akimiliki dhahabu nyingi , ufalme wake haukujulikana sana

Hatua hiyo ilibadilika wakati Mansa Musa ambaye alikuwa Muislamu aliamua kwenda Mecca kuhiji akipitia jangwa la Sahara na Misri.

Image captionSafari yake ya kuelekea Mecca ilisaidia kuiweka Mali katika ramani

Mfalme huyo aliripotiwa kuondoka Mali na msafara wa watu 60,000.

Alibeba ufalme wake wote na maafisa wake , wanajeshi, watumbuizaji , madereva wa ngamia na watumwa 12,000 mbali na idadi kubwa ya mbuzi , kondoo na chakula.

Ulikuwa mji uliokuwa ukipitia katika jangwa.

Mji ambao wakaazi wake hadi watumwa wake walikuwa wamevalia dhahabu na nguo za hariri.

Kulikuwa na ngamia 100 ambao kila mmojawao alikuwa akibeba mamia ya pauni za dhahabu.

Utajiri huo ulionekana zaidi wakati msafara huo ulipowasili mjini Cairo ambapo ulionekana.

Mvuto wa dhahabu mjini Cairo

Mansa Musa aliwacha hisia za kukumbukwa mjini Cairo hali ya kwamba al-Umar ambaye aliutembelea mji huo baada ya miaka 12 baada ya mfalme huyo wa Mali anakumbuka vile watu wa mji huo walimsifu mfalme huyo.

Aliwapatia watu dhahabu hali ya kwamba miezi yake mitatu mjini humo ilisababisha bei ya dhahabu kushuka thamani kwa kipindi cha miaka 10 hatua ilioharibu uchumi.

Kampuni ya kiteknolojia ya Marekani SmartAsset.com inakadiria kwamba kutokana na kuanguka kwa bei ya dhahabu, Hija ya Mansa Musa ilisababisha hasara ya $1.5bn (£1.1bn) katika uchumi wa eneo la mashariki ya kati.

Alipokuwa akirudi nyumbani, Mansa Musa alpitia tena Misri na kulingana wachache akajaribu kusaidia uchumi wa taifa hilo kwa kuondoa dhahabu iliokuwepo kupitia kuiomba kwa kiwango cha juu kutoka kwa wafanyibiashara wa Misri.

Wengine wanasema kuwa aligharamika sana hadi dhahabu alizokuwa nazo zikaisha. Lucy Duran wa Shule ya African and Oriental Studies mjini London anasema kwamba wanahistoria wa Mali walikasirishwa naye.

”Alitoa dhahabu nyingi ya Mali hali ambayo iliwafanya wanahistoria hao kutomsifu katika nyimbo zao na hadithi kwa kuwa wanaona kwamba alipoteza mali nyingi ya taifa hilo nje ya ufalme wake”, alisema.

Alipendelea sana Elimu

Hakuna shaka kwamba Mansa Musa alitumia ama kupoteza dhahabu nyingi wakati wa hija yake. Lakini ni kutokana na ukarimu wake wa kupitia kiasi ambapo alipata umaarufu duniani.

Mansa Musa aliiweka Mali na yeye mwenyewe katika ramani kisawasawa.

Katika ramani ya Catalan atlas kutoka mwaka 1375 , mchoro wa mfalme wa Afrika unaonekana umekalia ufamle wa dhahabu juu ya Timbuktu, akiwa ameshikilia kipande cha dhahabu mkononi.

Timbuktu ilikuwa eneo maarufu barani Afrika na watu walitoka maeneo ya mbali ili kujionea eneo hilo.

Katika karne ya 19, ilikuwa na kumbukumbu za kuwa mji uliopotoea na dhahabu duniani, ikiwa ni kielelezo cha Ulaya cha watafutaji na hiyo ilitokana na juhudi za Mansa Musa miaka 500 mapema.

Image captionMansa Musa aianzisha ujenzi wa msikiti wa Djinguereber mwaka 1327

Mansa Musa alirudi Mali kutolka Mecca na baadhi ya wasomi wa Kiislamu, ikiwemo jamaa wa mtume Muhammad.

Mwimbaji wa mashahiri na msanifu kwa jina Abu Es Haq es Saheli, ambaye anajulikana kwa kuchora mtindo wa msikiti wa Djinguereber .

Imeripotiwa kwamba mfalme huyo alimlipa mshairi huyo kilo 200 za dhahabu ambazo ni sawa na $8.2m (£6.3m). Mbali na sanaa na usanifu, alifadhili fasihi na ujenzi wa shule, maktaba na misikiti.

Na maramoja mji wa Timbuktu ukaimarika na kuwa kituo cha elimu na watu walisafiri kutoka maeneo mengine duniani ili kusoma katika kile ambacho baadaye kiliitwa Chuo kikuu cha Sankore.

Mfalme huyo tajiri alisifika kwa kuanzisha utamaduni wa elimu Afrika magharibi ijapokuwa hadithi hiyo ya Ufalme wake haina umaarufu mkubwa nje ya eneo la Afrika magharibi.

Historia huandikwa na wageni , kulingana na waziri mkuu wa vita vya dunia vya pili nchini Uingereza Winston Churchil.

Baada ya Mansa Musa kufariki 1337 akiwa na umri wa miaka 57 , ufalme huo ulirithiwa na wanawe wa kiume ambao walishindwa kuuleta pamoja .

Mataifa hayo madogo yalivunjika na ufalme ukaisha. Kuwasili kwa wazungu katika eneo hilo ndio kulipiga msumari wa mwisho ufalme huo.

Iwapo wazungu hao wangewasili mapema wakati wa utawala wa Musa , huku Mali ikisifika kwa jeshi lake kubwa na uwezo mambo pengine yangebadilika.

By Ally Juma.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents