Yafahamu maajabu haya ya mto Nile na sababu za maji ya mto huo kutumiwa na taifa la Misri tu pia ifahamu mito 10 mirefu zaidi duniani (+ Video)
Yafahamu maajabu haya ya mto Nile na sababu za maji ya mto huo kutumiwa na taifa la Misri tu pia ifahamu mito mirefu zaidi duniani (+ Video)
Mto Nile ni mto mkubwa upande wa bara la Afrika. Mara nyingi hutajwa kuwa pia ni mto mrefu kabisa duniani kushinda mto Amazonas. Kutoka Ziwa la Viktoria Nyanza hadi mdomo wake kwenye Bahari ya Mediteranea Nile inavuka nchi za Uganda, Sudan Kusini, Sudan na Misri kwa urefu wa km 6,650.
Beseni la Nile hukusanya maji ya eneo linalojumlisha 10% za eneo la Afrika yote au km²3,349,000. Takriban watu milioni 250 hukalia beseni hilo.
Chanzo cha Mto huu,
- Nile yenyewe (inaitwa pia Nile nyeupe) inayotoka katika Ziwa Viktoria Nyanza na
- Nile ya buluu inayotoka katika Ziwa Tana.
Majina hayo ya “nyeupe” na “buluu” yana asili yake katika mji wa Khartoum ambako mito yote miwili inaunganika ilhali kila mmoja una rangi tofauti kutokana na udongo tofauti uliotia rangi yake kwenye maji hayo. Vyanzo vya Nile ni mito yote inayopeleka maji kwenda Ziwa Viktoria Nyanza katika nchi za Tanzania, Burundi, Rwanda, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Uganda na Kenya. Chanzo cha mbali kabisa ni mto wa Luvironza huko Burundi unaoingia katika mto Kagera na kufika Ziwa Viktoria Nyanza. Mkono mwingine wa Nile unaanza Ethiopia ukiitwa Abbai au Nile ya Buluu: unatoka katika Ziwa Tana.
Hakuna mapatano kabisa Nile inaanzia wapi. Kawaida ya waandishi Waingereza ni kuhesabu kuanzia Ziwa Viktoria; waandishi wa mataifa mengine huwa wanaweza wakaita tayari mto Kagera kwa jina “Nile ya Kagera”.
Maji ya Nile.
Majina ya sehemu ya mto kuanzia Ziwa Viktoria hadi Khartoum ni kama yafuatayo:
- Nile ya Viktoria kuanzia Jinja inapotoka katika Ziwa Viktoria kwa km 500 hadi Ziwa Albert
- Nile ya Albert kuanzia Ziwa Albert hadi mpaka wa Sudan Kusini
- ndani ya Sudan Kusini mto huitwa Bahr al-Jabal (mto wa mlimani) hadi kupokea tawimto la Bahr al-Ghazal
- kwa sababu ya rangi wakati wa mvua yake kutokana na udongo katika maji jina linakuwa Bahr al-Abyad kuanzia Bahr al-Ghazal hadi Khartoum
- kuanzia Khartoum jina pekee ni Bahr an-Nil (mto wa Nile) hadi mdomo wake wa delta kwenye Mediteranea.
Matumizi ya Mto Nile.
Tangu milenia kadhaa maji ya Nile yamekuwa msingi wa maisha yote nchini Misri na pia kwa sehemu kubwa ya nchi ya Sudan.
Katika miaka ya 1920 Uingereza kama mtawala mkoloni wa Sudan na Misri ulikuwa na majadiliano juu ya ugawaji wa maji ya mto na kufikia mapatano juu ya matumizi ya maji ya mto Nile ya 1929.
Hadi leo Misri inadai ya kwamba mapatanao yale yanakataa ujenzi wa malambo na kuanzishwa kwa miradi ya umwagiliaji inayotumia maji ya Nile bila kibali cha serikali yake. Hapa Misri inadai ya kwamba nchi zote zilizokuwa makoloni ya Uingereza wakati ule zinafungwa na mapatano ya mwaka 1929 na hizi ni pamoja na Sudan, Uganda, Kenya, Tanzania, halafu pia Ethiopia iliyopatana na Uingereza wakati ule. Nchi nyingine hazikubali madai hayo, ila majadiliano juu ya mapatano mapya ya ushirikiano katika beseni la Nile yanaendelea.
Mito mirefu zaidi Du iani.
1. Amazon River – 6,853 km (4,325 miles) – America
2. Nile River – 6,853 km (4,258 miles) – Africa
3. Yangtze River – 6,300 km (3,917 miles) – Asia
4. Mississippi/Missouri – 6,275 km (3,902 miles) – Asia
5. Yenisei/Angara – 5,539 km (3,445 miles) – Asia
The 15 Longest Rivers in the World
Rank | River | Length (Miles) | Length (km) |
---|---|---|---|
1 | Amazon | 4,325 | 6,992 |
2 | Nile | 4,258 | 6,853 |
3 | Yangtze | 3,917 | 6,300 |
4 | Mississippi-Missouri | 3,902 | 6,275 |
5 | Yenisey-Angara | 3,445 | 5,539 |
6 | Yellow | 3,395 | 5,464 |
7 | Ob-Irtysh | 3,364 | 5,410 |
8 | Río de la Plata | 3,030 | 4,880 |
9 | Congo | 2,922 | 4,700 |
10 | Amur | 2,763 | 4,400 |
11 | Lena | 2,736 | 4,400 |
12 | Mekong | 2,705 | 4,350 |
13 | Mackenzie-Peace | 2,637 | 4,241 |
14 | Niger | 2,611 | 4,200 |
15 | Brahmaputra | 2,391 | 3,848 |
Mito mirefu ya Afrika inaonyeshwa katika orodha ifuatayo.
Mara nyingi mto wa Nile unahesabiwa kuwa mtu mrefu kuliko yote ya Afrika pia duniani. Kadirio la urefu wa mto hutegemea jinsi ya kuhesabu tawimito yake. Orodha inayofuata ina tofauti na orodha inayokadiria kwa namna nyingine.
Urefu (km) |
Jina | Mdomo | Beseni (km²) |
Kiasi cha maji kinachotolewa (m³/s) |
---|---|---|---|---|
6.671 | Nile pamoja na Kagera | Mediteranea | 3.071.306 | 2.832 |
4.835 | Kongo + Luvua pamoja na Luapula na Chambeshi | Atlantiki | 3.692.062 | 39.160 |
4.374 | Kongo | Atlantiki | 3.692.062 | 39.160 |
4.184 | Niger | Atlantiki | 2.112.774 | 9.570 |
2.574 | Zambezi | Bahari ya Hindi | 1.384.999 | 7.070 |
2.272 | Ubangi pamoja na Uele | Kongo | 613.202 | 7.000 |
2.160 | Oranje | Atlantiki | 941.421 | 800 |
2.153 | Kasai | Kongo | 925.172 | 10.000 |
1.820 | Shebeli | Juba | 336.627 | – |
1.819 | Volta pamoja na Volta nyeusi | Atlantiki | 414.243 | 1.290 |
1.800 | Okavango | inaishia katika delta ya barani ya Okavango | 721.258 | 0 |
1.740 | Chari pamoja na Ouham | Ziwa la Chad | 669.706 | – |
1.680 | Limpopo | Bahari ya Hindi | 414.524 | 800 |
1.658 | Juba | Bahari ya Hindi | 803.212 | 550 |
1.500 | Cuando | Zambezi | – | – |
1.450 | Lomami (mto) | Kongo | 110.000 | 1.700 |
1.430 | Senegal pamoja na Bafing | Atlantiki | 435.981 | 1.500 |
1.416 | Benue | Niger | 327.000 | – |
1.400 | Luvua pamoja na Luapula na Chambeshi | Kongo | – | – |
1.350 | Nile ya buluu (=Abay) | Nile | 326.400 | – |
1.288 | Shire pamoja na Songwe | Zambezi | – | – |
1.287 | Aruwimi | Kongo | 116.000 | – |
1.251 | Vaal | Oranje | 189.000 | – |
1.160 | Komoé | Atlantiki | 79.087 | – |
1.150 | Sankuru | Kasai | – | – |
1.140 | Volta nyeupe | Volta | – | – |
1.130 | Uele | Ubangi | – | – |
1.127 | Gambia | Atlantiki | 69.931 | 2.000 |
1.120 | Atbara | Nile | 100.000 | – |
1.100 | Kwango | Kasai | 263.500 | 2.700 |
1.100 | Sangha pamoja na Mambere | Kongo | 180.418 | – |
1.100 | Wadi Draa (mto wa muda) | Atlantiki | 114.569 | – |
1.094 | Ogooué | Atlantiki | 221.968 | – |
1.083 | Ruvuma | Bahari ya Hindi | 165.760 | – |
1.060 | Lukenie pamoja na Fimi | Kasai | – | – |
1.050 | Bani pamoja na Baoulé | Niger | – | – |
1.020 | Kunene 975 km? | Atlantiki | 110.024 | – |
1.000 | Kwilu 960 km? | Kwango | – | – |
1.000 | Molopo (mto wa muda) | Oranje (mto) | – | – |