Habari

Yaliyojiri kwenye kesi ya Maxence Melo mahakamani Kisutu

Kesi inayomkabili Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Jamii Media, Maxence Melo iliyokuwa isikilizwe Jumatatu hii katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam, imeahirishwa hadi Februari 16 mwaka huu kutokana na upelelezi wa kesi hiyo kutokamilika.

Uamuzi huo umetolewa na Wakili wa Jamhuri kudai kuwa upelelezi wa kesi hiyo bado unaendelea na haujakamilika bado, hivyo hakimu anayeendesha kesi hiyo Hakimu Mkazi Mkuu wa Kisutu, Victoria Nongwa aliutaka upande wa Jamhuri kukamilisha haraka upelelezi wa kesi hiyo ili iweze kusikilizwa tarehe iliyotajwa.

Kwa mujibu wa mtandao huo, Maxence Melo anashtakiwa kwa makosa mawili ikiwemo kuzuia Jeshi la Polisi kufanya uchunguzi kwa mujibu wa Sheria ya Makosa ya Mtandao na Kusajili tovuti ya JamiiForum kwa kikoa cha .com badala ya .co.tz jambo ambalo inadaiwa ni kinyume cha sheria.

BY: Emmy Mwaipopo

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents