Michezo

Yanga SC yamvamia mnyama ‘Simba SC’ kileleni VPL

Mabingwa wa kihistoria wa ligi kuu ya Vodacom Tanzania Bara, Dar es Salaam Young Africans imefanikiwa kupata pointi tatu muhimi dhidi ya timu ya Stand United baada ya kuchomoza na ushindi wa mabao 3 – 1 mchezo uliyopigwa Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Mabao ya mabingwa hao watetezi yamefungwa na Mhilu na Ajibu katika kipindi cha kwanza na Obrey Chirwa akihitimisha mabao matatu kipindi cha pili huku kwa upande wa Stand United likifungwa na Vitalis Mayanga.

Kwa matokeo hayo unaifanya Yanga SC kuwa na jumla ya alama 46 sawa na vinara Simba SC wakiwa na tofauti ya magoli ya kufungwa na kufunga.

Related Articles

Check Also
Close
Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents