Michezo

Yanga SC yatangaza kuanza na Tv kisha Radio

Uongozi wa klabu ya Yanga umetangaza kuanzisha vipindi vya michezo vitakavyo ruka katika luninga ya Azam TV kama ilivyo kwa mahasimu wao Simba SC ambao wao tayari walishaanza pamoja na timu ya Azam FC.

Wakiongea na waandishi wa habari katibu mkuu wa klabu ya Yanga, Charles Boniface Mkwasa  na meneja wa vipindi wa Azam Tv, Baruani Muhuza wamesema kuwa vipindi hivyo vitakuwa na utafauti mkubwa na vile vya klabu za Simba na Azam FC kwakuwa vitakuwa vikizalishwa katika studio za hapo klabuni na kunamatarajio ya kuanzisha na kituo cha radio.

Yanga inatarajia kuzindua rasmi vipindi hivyo vya michezo ambavyo vitakuwa vikizalishwa hapo makao makuu Jangwani mwezi ujao na hivyo watangazaji watakuwa ni wana Yanga wenyewe.

Wakati huo huo uongozi ya wanajangwani hao umeingia mkataba na mtandao wa simu za mkononi Tigo ambao watawezesha wanayanga na wapenzi wa soka kwa ujumla kupata  habari kupitia ujumbe mfupi wa njia ya simu ‘SMS’.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents