Michezo
Yanga yaagizwa kutoa Tamko kwa kocha, Mrisho Ngasa, Kabwili wafungiwa, Njombe Mji waingia 7 Uwanjani (+Video)
Kamati ya Uendeshaji na Usimamizi wa Ligi Kuu Tanzania Bara (Kamati ya Saa 72) imemuonya Kocha Mkuu wa Klabu ya Yanga, Luc Eymael kwa kufuatia kufanya vitendo na kutoa kauli zisizofaa kwenye mchezo namba 89, baina ya Azam FC dhidi ya Yanga SC hata hivyo imeitaka timu hiyo itowe tamko mara moja juu ya kauli zake za kibaguzi.
Kamati hiyo ya saa 72, pia imetaja baadhi ya matukio mengine ambayo waliyapitia na kutoa adhabu ikiwa ni pamoja na baadhi ya wachezaji kama Mrisho Ngasa kwa kosa la kugoma kuingia vyumbani.