Michezo
Yanga yainyuka Al Ahly ya Misri bao 1 – 0
Nadir Haroub Kanavaro Jumamosi hii ameitoa kimasomaso Yanga kwa kuifungia bao moja na la ushindi dhidi ya klabu ya Al Ahly ya Misri kwenye mechi iliyofanyika kwenye uwanja wa taifa jijini Dar es Salaam.
Hiyo ilikuwa ni mechi ya kwanza kati ya timu hizo kwenye hatua ya timu 32 ya mabingwa wa Afrika. Nadir alifunga bao hilo katika dakika ya 82, dakika tu 8 kabla ya kumalizika kwa mechi hiyo.
Mechi ya pili kati ya timu hizo itachezwa Jumapili ijayo jijini Cairo, Misri. Hata hivyo mchezo huo uliingia matatani kipindi cha pili baada ya mashabiki kurusha chupa uwanjani.