Burudani

Young Dee aibukia kwenye muziki wa Gospel, mwenyewe aeleza namna alivyopokea upako kupitia simulizi hii

Tarajia kusikia wimbo wa Injili kutoka Rapa Young Dee kwani tayari mwenyewe ameeleza namna alivyoguswa kupitia simulizi ya kusisimua aliyoiweka kwenye ukurasa wake wa Instagram.

Young Dee

Young Dee akieleza wimbo huo alioutunga tayari, amesema kuwa atamshirikisha Ben Pol na utakuwa ni wimbo wa kumshukuru Mungu.

Leo nimeskia story moja imenigusa sana! Nmeona kuna kila sababu ya kumshukuru Mungu kila uionapo siku mpya..!! Kuna mtu alipata mshtuko na kupoteza uwezo wa kupumua kwa ukawaida ikabidi apewe huduma ya kupumua kwa mashine (Oxygen) kwa Muda wa Masaa nane.. baada ya kupata nafuu na kupona akatolewa chumba cha wagonjwa mahututi kisha kuandikiwa gharama zake za matibabu yale ambayo ilifika kiasi cha Pounds 5000 sawa na Tshs.14, 870,186 (Milioni kumi na nne laki nane na ushee hivii).. baada ya kupewa hiyo bill akaanza kulia… Haikua rahisi kuelewa kwanini analia kulingana na uwezo wake kifedha maana ni mtu anaejiweza, ila alichoongea ndio kimenifanya kushare na wewe hii story!! Ni kwamba aliwaza kwa umri wake wote wa miaka 70 amekua akipumua bila gharama yoyote lakini kwa masaa nane tu imemgharimu kiasi hiko cha pesa je? Angedaiwa pumzi na M/mungu hadi leo hii ingekuwaje? Je unajua thamani ya pumzi yako kabla hujamuomba chochote Muumba wako?🤔 Hapa mimi Nawaza kuandika ngoma moja ya kumsifu yeye muweza wa yote aisee #Amgrateful🙏🏽 Oi @iambenpol Niandalie chorous Baller

Hata hivyo, bado haijaeleweka kama atahamia kwenye Gospel moja kwa moja au utakuwa ni wimbo wa Inspiration kama wanavyofanya wasanii wengine wa Bongo Fleva.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents