Burudani
Young Dee awataka wasanii kuachana kuoneana wivu
Rapper Young Dee amewataka wasanii wenzake kuacha kuoneana wivu baina yao kwa kuwa wote wanatafuta riziki kupitia muziki.
Young Dee aliiambia Planet Bongo ya EA Radio jana kuwa wasanii wanatakiwa kuombeana dua kwa kuwa wote ni wamoja. “Mimi huwa naamini kwamba as long as wote tunatafuta ugali kwa kutumia mic haina haja ya kuoneana jealous,” alisema.
“Ni kuombea tu heri kila mtu afanikiwe katika sehemu yake anayofanya. Mimi ni Young Dee na wengine wana majina yao na kila mtu ana brand yake kama msanii,” alisisitiza.