Burudani
Yvonne Chaka Chaka, Mafikizolo na Sauti Sol kutumbuiza Dar June 6
Muimbaji mkongwe wa Afrika Kusini, Yvonne Chaka Chaka pamoja na kundi la Mafikizolo watatumbuiza jijini Dar es Salaam, June 6 mwaka huu.
Show hiyo imepewa jina la Party In The Park – SA Invasion ambapo pamoja na wasanii hao, kundi la nchini Kenya, Sauti Sol nalo litakuwepo kutumbuiza.
Wasanii wengine ni pamoja na Black Motion, Zaki Ibrahim Beatenberg Xoli na Michael Djvoodoosa Darcio.