Burudani
Z-Anto kurudi Tip Top?
Kijana aliyepata kufanya vyema kunako game ya muziki wa kizazi kipya, Z-Anto juzi kati alionesha dalili za kurudi ndani ya kundi lililomtoa, Tip Top Connection baada ya kudandia stejini na kusapoti uzinduzi wa kundi hilo uliyopigwa ndani ya Club Sun Cirro iliyopo pande za Sinza, Dar.
Ilikuwa kama ‘surprise’ wakati MC wa shughuli hiyo, Mwalubadu alipomtaja Z-Anto kuwa anapanda stejini na kusapoti uzinduzi huo, wengi hawakuamini kwakuwa ‘dogo’ aliondoka kundini kwa jazaba huku akianika madai yake kwa viongozi wa Tip Top kunako vyombo kadhaa vya habari.
Kwa sasa bongo5.com ipo katika harakati za kuwasiliana na uongozi wa Tip Top Connection kupata habari zaidi juu ya hili swala.