Michezo

Zaidi ya mashabiki 100 wa Uingereza wakamatwa na polisi

Zaidi ya mashabiki miamoja wa Uingereza wametiwa mbaroni siku ya Ijumaa huko Amsterdam wakiwa wanakwenda kuishabikia timu yao ya taifa iliyokuwa na mchezo wake wakirafiki dhidi ya Netherlands.

Idadi hiyo ya mashabiki waliyo kamatwa ni ya siku mbili baada ya wengine 25 kukamatwa siku ya Alhamisi.

Askari Polisi wamesema kuwa mashabiki hao walikuwa wakihatarisha amani ya nchi baada ya kuwashafataki mitaani.

Katika mchezo huo wa kirafiki timu ya taifa ya Uingereza iliibuka na ushindi wa bao 1 – 0 dhidi ya Netherlands lililofungwa na Lingard.

Zaidi ya mashabiki 5,234 kutoka nchini Uingereza walikadiriwa kuwepo katika mchezo huo wa krafiki Amsterdam Arena hapo jana siku ya Ijumaa.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents