Burudani

Zari athibitisha Wema Sepetu ndiye amevunja mahusiano yake na Diamond

Unazikumbuka picha za Wema Sepetu na Diamond Platnumz zilizosambaa wakiwa wamekumbatiana kwa mahaba wakati wa sherehe ya kumkaribisha Maromboso au ‘Mbosso’ iliyofanyika mwezi uliopita katika hoteli ya Hyatt Regency Dar es Salaam?

Basi tukio lile ndio limesababisha Diamond kuweza kupigwa chini na mama watoto wake, Zari The Bosslady.

Akiongea katika kipindi cha runinga cha Dira ya Dunia ya BBC Swahili, Zari amesema, “Tulikuwa tunajaribu kuona we can move from hiyo sikendo ya kupata mtoto. So we can move forward lakini vitu kama hivyo leo unasikia hivi unaona vile sijui kukumbatiana huko na maex kwenye public vitu vya kunidhalilisha, kunifanya niwe very disrespect na watoto wangu unaona tu like it’s just not right.”

Zari ameongeza kuwa Diamond hakuwahi kumueleza chochote kuhusu picha hizo na wala yeye hakuwahi kumuuliza kwa kuwa aliona haina maana kwake.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents