Michezo

Zidane atimka kambini Montreal, akitelekeza kikosi cha Real Madrid

Kocha Mkuu wa Real Madrid, Zinedine Zidane ameondoka kambini mchana wa leo na kurejea nyumbani huku akikiacha kikosi cha miamba hiyo ya soka Hispania kikiwa na wasaidizi wake huko Montreal.

Zinedine Zidane has left Real Madrid's pre-season camp in Montreal on Friday afternoon

Imeelezwa kuwa sababu binafsi ndiyo chanzo cha kurejea nyumbani huku akikiacha kikosi hicho kikiwa katika ‘personal reasons’ kwaajili ya ligi kuu Hispania na mashindano mengine.

Mfaransa huyo aliwasili huko Canada na kikosi chake mapema wiki hii, huku kikiwa na wachezaji wengi wenye majina makubwa kama maandalizi ya kuelekea Marekani katika michuano ya  International Champions Cup mapema mwezi ujao.

Taarifa za ndani ya klabu hiyo zinaeleza kuwa “Kocha wetu, Zinedine Zidane ameondoka kambini huko Montreal kwa sababu ya mambo binafsi.” Imeeleza Real Madrid

“Hadi hapo atakapo rudi, kwa sasa mazoezi yanasimamiwa na kocha msaidizi, David Bettoni.”

Zidane has now handed first-team responsibilities over to his No 2 David Bettoni

Real itakabiliana na Bayern Munich Julai 21 kabla ya kukutana na Arsenal pamoja na Atletico Madrid mwishoni mwa mwezi. Miamba hiyo ya Liga pia itacheza na Tottenham kwenye kombe la Audi Cup.

Kocha huyo mwenye umri wa miaka 47, amefanikiwa kumsajili Eden Hazard akitokea Chelsea kwa dau la pauni milioni 150. Mshambuliaji, Luka Jovic na Rodrygo wamewasili pamoja na beki, Ferland Mendy na Eder Militao.

Related Articles

Check Also
Close
Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents