Zidane kurudi kazini hivi punde, atangaza kutua Old Trafford na wachezaji hawa hatari
Zinedine Zidane amethibitisha kuwa muda si mrefu anarejea kwenye maisha ya soka na kuendelea kufundisha licha ya kuwaacha watu na maswali ni klabu gani ataelekea.
Kiungo huyo wa zamani wa Ufaransa amekuwa nje ya majukumu ya soka tangu alipotangaza kuacha kukinoa kikosi cha Real Madrid baada ya kuwepo hapo Los Blancos kwa mafanikio makubwa.
Kwa mara ya kwanza amekiambia chombo cha habari nchini Hispania, TVE kuwa anampango wa kurudi hivi karibuni kwakuwa ndiyo kitu anachokipenda.
Zidane angependa kuchukua nafasi ya Jose Mourinho endapo Mreno huyo angetimuliwa ndani ya Manchester United. Mwezi uliyopita aliwahi kumuambia rafiki yake kuwa anatarajia kupata ofa kutoka Old Trafford.
Kwa sasa Mourinho yupo kwenye presha kubwa baada ya kushindwa kufanya vizuri katika dirisha la usajili lililopita na kupoteza michezo miwili kati ya minne ya ufunguzi wa pazia ya ligi kuu England.
Zidane ametangaza kuwasajili, Toni Kroos, Thiago Alcantara, James Rodriguez na Edinson Cavani endapo dili lake la kutua Manchester litatimia.