Zilla kuja na Ally K
Msanii wa muziki wa kizazi kipya Golden Jacob Mbunda amesema kwa sasa amejipanga kuja na ujio mpya na wimbo mpya utakao itwa Milele ambao amemshirikisha mwanamuziki Ally Kiba, katika wimbo huo ambao amesema utakuwa na milindo ya kiasili kidogo iliyochanganywa.
mwanamuziki Zilla amesema kazi hiyo yote imefanyika chini ya mkali Marco Challi, huku video yake ikigongwa na Adamu Juma. amesema ni miongoni mwa video ambayo itakuja kuwashika watu katika msimu huuu, na ndiyo itakuwa ya kwanza kabla ya Audio ya wimbo huo.
GodZilla akiwa na Ezza Challi maarufu kama Zachaa kiongozi na meneja wa kundi la Young Chalz.
Hapa Godzilla akiwa na mdau wa Bongo5, Mo One’s
Zilla amesema baada ya kufanya kazi hizo na Ally K, anatarajia kuachia albamu yake itakayokwenda kwa jina la KINGDOM ZILLA’ ambayo itakuwa na nyimbo kumi zilizoshiba, huku ikiongozwa na Salasala, pamoja Kingdo.