BurudaniDiamond Platnumz

Zinaweza zikafungiwa nyimbo zetu zikachezwa za kina Nicki Minaj – Diamond

Msanii Diamond Platnumz bado anaonekana kutokubaliana na uamuzi wa Mamlaka ya Mawasiliano Nchini (TCRA) wa kuzifungia nyimbo zake mbili ambazo ni Waka na Hallelujah.

Muimbaji huyo akizungumza na Classic FM nchini Kenya amesema serikali ni lazima iangalie maudhui ya wimbo husika na msanii husika nini hasa alilenga.

“Huwezi kuimba nyimbo za mapenzi usitaje maneno ya kimahaba, ni uongo kwa sababu utakuwa haufikishi ujumbe,” amesema.

“Nyimbo kama Waka na Hallelujah ni nyimbo ambazo nilifikiria kufanya kitu ili soko lingine watusikilize, serikali lazima ielewe. Na kinachouma zaidi zinaweza zikafungiwa nyimbo zetu zikachezwa za kina Nick Minaj, so ni lazima tuangalie,” amesisitiza Diamond.

February 28 mwaka huu Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) ilipokea list ya nyimbo 15 zisizokuwa na maadili kutoka kwa Baraza la Sanaa Taifa (BASATA) na kuamuru kutopigwa katika vyombo vya habari. Katika list hiyo Nay wa Mitego alifungiwa nyimbo tatu na Diamond nyimbo mbili.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents