Habari
Zitto awashauri Watanzania wasimamishe shughuli zao kwa dakika moja ifikapo saa 7 mchana
Mbunge wa Kigoma Mjini, Mhe. Zitto Kabwe amewashauri Watanzania kusimamisha shughuli zao kwa dakika moja ifikapo saa 7 mchana leo Septemba 7, 2018 ili kumuombea Mbunge wa Singida Mashariki, Mhe. Tundu Lissu anayepatiwa matibabu nchini Ubelgiji.
Zitto ametoa ushauri huo kupitia ukurasa wake wa Twitter, ikiwa leo ni mwaka mmoja umepita tangu Lissu ashambuliwe kwa risasi jijini Dodoma Septemba 7, 2018 majira ya saa 7 mchana akitokea bungeni kwenda nyumbani kwake Area D.