Zitto Kabwe amjibu Bashe baada ya kukaribishwa CCM ‘Wajibu niliyojipa duniani ni kuiua CCM’
Mbunge wa Nzega Mjini kupitia chama cha Mapinduzi (CCM), Hussein Bashe amemkaribisha ndani ya chama hicho mbunge wa Kigoma Mjini kwa tiketi ya ACT Wazalendo, Zitto Kabwe hii ni mara baada ya aliyekuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Uongozi ya CUF, Julius Mtatiro kutangaza adhima yake ya kuachana na CUF.
Mbunge wa Nzega Mjini kupitia chama cha Mapinduzi (CCM), Hussein Bashe
Mara baada ya Zitto Kabwe kuponda hatua ya Mtatiro kujivua uanachama wa CUF na kutangaza nia ya kujiunga na CCM. kupitia ukurasa wake wa Twitter akiandika ”Mwingine naye amejitoa kwa sababu zile zile hewa.”
Mbunge wa Kigoma Mjini kwa tiketi ya ACT Wazalendo, Zitto Kabwe
Ndipo Bashe akatumia nafasi hiyo kumkaribisha Zitto kujiunga na chama hicho cha Mapinduzi CCM ”Kaka na ndugu yangu Zitto Kabwe karibu CCM, wakati mwingine ni rahisi kuleta mabadiliko ya haki, demokrasia na maendelei ukitokea ndani ya CCM kuliko kuyatafuta nje.”
Naye Mh Zitto akajibu kuwa ”Wajibu nimejipa duniani ni kuiua CCM ili kukata mnyororo wa ‘underdevelopment” nchini kwetu. Nikishindwa mimi watafanya kizazi kijacho Lakini CCM itatoka tu. Hakuna marefu yasiyo na ncha.”
Kaka na Ndg yangu@zittokabwe, karibu CCM Sometimes its easy kuleta mabadiliko ya Haki,demokrasia,na maendeleo from within CCM kuliko kutafuta Reforms from outside bcs there is ideological,Structural and Moral Crisis huko nje few true solders out there
— Hussein M Bashe (@HusseinBashe) August 11, 2018
Wajibu nimejipa duniani ni ku destroy CCM ili kukata mnyororo wa underdevelopment nchini kwetu. Nikishindwa mimi watafanya kizazi kijacho Lakini CCM itatoka tu. Hakuna marefu yasiyo na ncha
— Zitto MwamiRuyagwa Kabwe (@zittokabwe) August 11, 2018
Mmm,mazima ayo kaka ZITTO, ,aho wako apo kwa masilai ya biashara zao na kuogopa kunyanyaswa wakijikuta wako mnje ya CCM,usizani atujui sisi,
Umechelewaaaa
Atakufa yeye asipoangalia. Au atakuwa kama Lowassa. Akingojea kuwa Rais wa nchi
Mmh labda ufe ww lakin kwa ccm tena jina sio mtu kama unavyosema ww manae ccm haijulikan mwenyewe ni nan watu wanaiyona ipo naitaendelea kuwepo mababu na mabibi wamewacha sembuse ww ndugu yangu angalia tu familia yako siasa haina kwao ndomana kuna watu wana uwezo ila hawawaz siasa kabisa kwanza yatia ugonjwa wa moyo kwa upeo rabda makufuli anastarehe kag zaid yakupewa maneno machafu ataman leo akivue hicho cheo hana jins tu kama vip unda kampen yakusaidia watoto yatima upate swawabu itakua her kuna watoto wanahaha tu mitaan hawajui pakushika
Kwa hilp tupo pampja hadi kieleweke!! Nakukubali sana zito
Sasa kapuku ongea hiyo kauri ya zito uone kama ujakutana na binadamu wasiojulikana
Kabla haijafa CCM itakufa ACT Wazalendo ambayo kwa sasa upo mahututi kwa ufupi ipo ICU
Watahama sana kwenda ccm kwa sasa mh Z lkn upo muda watatoka wengi.
Zito ni mtopokaji