Habari
Zitto Kabwe atolewa Oysterbay apelekwa Central Polisi kuhojiwa zaidi, uchochezi watajwa (+video)
Baada ya kuhojiwa kwa takribani saa nne katika kutuo cha polisi Oysterbay jijini hapa, Mbunge wa Kigoma Mjini na Kiongozi wa ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe amehamishiwa Kituo Kikuu cha Polisi kwa mahojiano zaidi.
Akiongea na Waandishi wa Habari muda mfupi baada ya Zitto kutolewa kituo cha Oysterbay, Katibu Mwenezi wa ACT Wazalendo amesema kuwa kiongozi wao anaenda kuhojiwa zaidi kwa tuhuma za uchochezi.