Afisa Habari mpya wa Klabu ya Yanga, Ally Kamwe amesema kuwa wapinzani wao kwenye mchezo wa Ligi ya Mabingwa, Al Hilal ni timu ndogo sana tofauti na inavyozungumziwa na wachambuzi wa soka.
Ally Kamwe ameyasema hayo kupitiwa Wasafi fm, Yanga itashuka kwenye uwanja wa Mkapa Oktoba 8, 2022 kukabiliana na timu hiyo kutoka Sudan.