Siasa

Alpha Conde aachiliwa kutoka kifungo cha nyumbani 

Rais wa zamani wa Guinea Alpha Conde ameachiliwa kutoka kifungo cha nyumbani zaidi ya miezi saba baada ya kuondolewa madarakani katika mapinduzi ya kijeshi, serikali ya mpito ilisema kwenye televisheni ya taifa siku ya Ijumaa.

Conde, mwenye umri wa miaka 84, alikuwa kizuizini tangu Septemba mwaka jana, wakati wanajeshi wa kikosi maalum walipompindua kwa madai ya kuendeleza ufisadi wa serikali.

Serikali mpya ya kijeshi ya Guinea imemruhusu Conde kupokea wageni, na mapema mwezi huu ilimruhusu kusafiri hadi Umoja wa Falme za Kiarabu kwa ajili ya kuchunguzwa afya yake.

Ataendelea kuishi katika nyumba ya familia ya mke wake katika kitongoji cha mji mkuu Conakry hadi ukarabati wa nyumba yake utakapokamilika, serikali ya mpito ilisema katika taarifa yake.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents