FahamuHabari

Anusurika kifo baada ya kushambuliwa na chatu kwenye bwawa la kuogelea

Mvulana mwenye umri wa miaka mitano raia wa Australia amenusurika kifo baada ya kubanwa na kuangushwa kwenye bwawa la kuogelea na chatu urefu wa mita 3 sawa na futi 10 ambaye alikua na ukubwa wa takriban mara tatu ya umbo  la kijana huyo.

Beau mwenye umri wa miaka mitano alikuwa akicheza kando ya bwawa huko Byron Bay wakati chatu mwenye urefu wa mita tatu (futi 10) alipompiga kutoka kwenye mimea ya karibu, babake Ben Blake aliiambia redio ya Tisa siku ya Ijumaa.

“Ninaamini chatu alikuwa ameketi pale akingojea mwathiriwa aje, Chatu alimng’ata mtoto, akatumbukia ndani ya maji na kujisonga karibu na mguu.

Babu wa mvulana mwenye umri wa miaka 76 alijirusha kwenye bwawa, akapiga mbizi ndani ya bwawa na kumwinua mvulana huyo nje – huku nyoka akiwa bado ameshikamana.

“Mimi sio mvulana mdogo, nilimfanya aachiliwe ndani ya sekunde 15-20,” aliambia kituo cha redio.

Related Articles

Check Also
Close
Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents