Michezo

Arsenal yamuomba, Arthur Melo kwa mkopo

Arsenal wamefanya mawasiliano na Juventus kuhusu mkataba wa mkopo wa kiungo wa kati wa Brazil Arthur Melo, 25. Pia wanamlenga kiungo wa kati wa Leicester na Ubelgiji Youri Tielemans, 24. (Goal)

Arsenal set to sign £72m star who 'surprised' Messi, negotiations advanced

The Gunners pia bado wanavutiwa na mshambuliaji wa Fiorentina Dusan Vlahovic, 21, lakini watakuwa na shida kufadhili uhamisho wa Mserbia huyo kufikia mwisho wa mwezi. (Sky Sports)

Wakati huo huo meneja wa PSG Mauricio Pochettino bado anawasiliana na Man Utd kuhusu uhamisho wa majira ya joto. Meneja wa sasa wa muda Ralf Rangnick, hata hivyo, anamtaka bosi wa Ajax Erik ten Hag. (Le Parisien, via Sun)

th

Beki wa Chelsea Antonio Rudiger sasa anapanga kusalia Stamford Bridge. Mjerumani huyo, 28, ambaye mkataba wake unamalizika msimu ujao alikuwa akihusishwa na kutaka kuondoka. (Bild, via Teamtalk)

Aston Villa wanawinda saini ya kiungo wa kati wa Brighton Yves Bissouma, 25(Telegraph)

Leicester City na Filip Benkovic wamekubali kufuta kandarasi ya beki huyo wa Croatia mwenye umri wa miaka 24. (Leicester Mercury)

th

Ousmane Dembele anatazamiwa kuondoka Barcelona mwishoni mwa msimu huu na Manchester United wanamtaka mchezaji huyo wa kimataifa wa Ufaransa mwenye umri wa miaka 24. (Mirror)

Tottenham wamekataa ombi la winga wa Uholanzi Steven Bergwijn, 24, kutoka Ajax. (Talksport)

Newcastle wanatayarisha ofa ya kumnunua kiungo wa kati wa RB Leipzig na Mali Amadou Haidara, 23. (Mail)

Tottenham wanataka kusajili wachezaji watatu muhimu katika dirisha la uhamisho. Spurs wako kwenye mazungumzo na Wolves kuhusu kiungo wa kati wa Uhispania Adama Traore, 25, na wanatafuta beki wa kulia na mshambuliaji. (Telegraph)

Leeds wanavutiwa na beki wa pembeni wa Torino na Nigeria Ola Aina, 25(Calciomercato – in Italian)

Related Articles

Check Also
Close
Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents