Habari
Bajeti ya fedha mwaka 2021/22 kufikishwa bungeni, ni ya kwanza kwa serikali ya awamu ya sita
Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Mwigulu Nchemba, leo saa kumi alasiri atawasilisha bajeti Kuu ya Serikali kwa mwaka wa fedha wa 2021/2022 Bungeni jijini Dodoma.
Bajeti hiyo ni ya kwanza, tangu Serikali ya awamu ya sita ilipoingia madarakani.