Chadema waeleza kuwa Mbowe hajulikani alipo
Kiongozi wa upinzani nchini Tanzania Freeman Mbowe ameripotiwa hajulikani alipo katika chumba chake cha hoteli jijini Mwanza.
Taarifa kupitia ukurasa wao wa Twitter inaeleza kuwa Bw Mbowe huenda amekamatwa alipokuwa akihudhuria mkutano wa chama chake cha Chadema.
Hatahivyo polisi haijatoa tamko lolote kuhusiana na taarifa za kukamatwa kwake
Maafisa kutoka chama chake wanasema kuwa hadi sasa hawajaweza kubaini anashikiliwa kwenye kituo kipi cha polisi.
Kulingana na taarifa ya Chadema iliyotumwa kupitia akaunti yake ya Twitter, Bw Mbowe amekamatwa pamoja na wanachama wengine 10 wa chama hicho.
Mwenyekiti CHADEMA Taifa @freemanmbowetz haijulikani alipo baada ya Jeshi la Polisi kuvamia hoteli aliyofikia na kuwakamata na viongozi wengine wamepelekwa Kituo cha Kati, Mwanza lakini Mwenyekiti hajulikani alipo. pic.twitter.com/TIBP51nHFu
— CHADEMA Tanzania (@ChademaTz) July 21, 2021