
Chelsea FC itakuwa Klabu ya kwanza kutoka Premier League kuandaa Futari kwaajili ya Waislamu watakao kuwa kwenye Mfungo wa Mwezi Mkukufu wa Ramadhan.
Tukio hilo la kihistoria litafanyika Machi 26, kwenye Uwanja wa Stamford Bridge lengo likiwa ni kukuza uvumilivu wa kidini na kuleta umoja.
Kufuturisha wakati wa Ramadhan litakuwa ni tukio kubwa zaidi katika jamii ya Uingereza, itaruhusu Waislamu kukusanyika na kufungua mfungo wao pamoja.
Hafla hiyo itahusisha Misikiti ya karibu na Klabu hiyo, Wanachama na Wafanyakazi wa Chelsea wa imani ya Kiislamu, itawaleta watu pamoja na kukuza uelewa wa Ramadhan.
Imeandikwa na @fumo255