Michezo

Chelsea kumrejesha Lukaku EPL

Chelsea wanajiandaa kutoa ofa ya pauni milioni 86.3 kwa ajili ya mshambuliaji Mbelgiji anayecheza katika klabu ya Inter Milan Romelu Lukaku, 27, endapo the Blues watashindwa kumsajili mshambuliaji Erling Braut Haaland,20, wa Borussia Dortmund (Calciomercato-in Italian)

Romelu Lukaku

Tottenham watajaribu kumsajili mlinzi wa kati wa Southampton Jannik Vestergaard,28, mwenya thamani ya pauni milioni 18, baada ya dirisha la usajili kufunguliwa. (Express)

Liverpool wameiambia RB Leipzig kuwa hawatamsajili mlinzi wa kati, Mfaransa Ibrahima Konate,21, (Bild, via Express)Ibrahima Konate

 Liverpool imesitisha mpango wa kumsajili mlinzi wa RB Leipzig Ibrahima Konate

Reds watakabiliwa na ushindani wa Chelsea katika kumnasa kiungo wa kati wa Ajax Ryan Gravenberch,18, ambaye anatazamwa kuwa mbadala wa Georginio Wijnaldum,30. (Gazzetta dello Sport,via Express)

Manchester City wanalenga kukubaliana kuingia mkataba mpya nawashambuliaji wa England Phil Foden,20, na Raheem Sterling,26, kabla ya mwishoni mwa msimu, baada ya kiungo wa kati wa Ubelgiji Kevin de Bruyne,29, kuongeza mkataba wake wa mpaka mwaka 2025. (Eurosport)

Manchester City haitamfuatilia mshambuliaji wa Argentina Lionel Messi mpaka mchezaji huyo, 33, atakapoweka wazi kuwa anataka kuondoka Barcelona. (Marca-in Spanish)

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents