Burudani

Diamond atajwa katika vipengele 7, ngoma ya Waah yambeba (+ Video)

Msanii wa Tanzania , Diamond Platnumz ametajwa vipengele vingi katika tuzo za Afrima zitazofanyika Novemba mwaka huu nchini Nigeria.


Orodha ya wateule wa tuzo hizo imeanikwa jana Jumatano Septemba 22,2021, ambapo wasanii wengi kutoka Tanzania wakiingia katika vipengele 13, huku Diamond akijitokeza kwenye vipengele vingi zaidi ya wengine.
Kwa upande wa Diamond wimbo wa Waah! ndio umembeba, kwani licha ya kumuingiza katika vipengele vinne pia umetajwa katika vipengele saba vikiwemo wimbo bora wa mwaka, video bora ya mwaka, wimbo unaochezeka na wimbo bora wa kushirikiana. Pia Waah! Umeingia katika vipengele vya msanii bora wa mwaka na msanii bora wa kiume Afrika Mashariki.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents