Burudani
Diamond atamsusa D voice wakija wasanii wapya WCB!!

Kupitia kwenye kipindi chake cha RECAP & MANDO @el_mando_tz ameizungumzia ngoma mpya ya D Voice kutoka WCB ya Mbwa.
Anasema ni kweli D Voice ameamua kubadilika kutoka Singeli na sasa Bongo Fleva lakini bado kuna kazi kubwa ya kufanya ili kufika mbali zaidi.
Anasema kila mwaka inaonekana D Voice yule yule na mwaka huu WCB wametangaza kusaini wasanii wengine inaweza kuja kuwa hatari sana kwa D Voice.
Anasema Pressure kwake itaongezeka na ukiangalia kwenye muziki bado hajasimama pekee yake, wasanii wakija wapya Upepo wote utahamia kwao.
Swali linakuja D Voice ameweza kusimama kama ilivyokuwa Zuchu na Mbosso?? Attention anayopewa na Boss wake pamoja na lebo itakuwa ile ile au itapungua??