
Makamu Mwenyekiti Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo @ChademaTz John Heche @hechejohn amehoji juu ya kukamatwa na kunyimwa dhamana kwa aliyekuwa Katibu Mkuu wa chama hicho Dkt. Wilbroad Slaa na pia endapo akifariki taarifa itakayotolewa itakuwa ya aina gani.

“Mzee kama Dkt. Slaa mzee wa miaka 76 amekuwa mbunge kwa miaka 15, amekuwa Katibu Mkuu wa CHADEMA amekuwa Balozi, unamkamata kesi ambayo ina dhamana unatumia mahakama kumuangamiza, hivi akikufia Rais Samia @SuluhuSamia unamtoaje unatuambiaje watu? kwamba amekufa tu kifo cha kawaida, leo wakakuambia Dkt. Slaa hatupo naye tena unawaambiaje watanzania”
Heche ameyasema hayo Februari 12, kwenye mkutano wake wa hadhara Sirari, jimbo la Tarime vijijini.
cc:Jambo Tv