Muziki

Dogo Janja aachia album yake ambayo ameshirikisha wasanii wa kike zaidi #AsanteMama

Msanii wa muzikiBongofleva  kutoka lebo ya Madee MMB Dogo Janja hatimaye amewaka kiu mashabiki wake baada ya kuidondosha Rasmi album iliyokuwa ikisubiriwa kwa hamu inayokwenda kwa jina la  #AsanteMama

Album hii ina jumla ya ngoma 11 ambapo Ngoma 10 kati ya hizo Janjaro ameshirikishwa ma-star wa kike tu, Baadhi ya mastaa hao ambao wameshirikishwa ni pamoja na  @officialnandy @jidejaydee @officialkhadijakopa @rosa_ree @mauasama @officiallinah @luludivatz @mimi_mvrs11 pamoja na @patrisiahillary

Huku kwenye bonus track kwenye album hiyo amewashirikisha ma-star wa kiume kutokea nchini Uganda 🇺🇬 waliokua wanaunda Kundi la Muziki la #GoodLyfe @radioandweasel na Wimbo huu ni #MyLifeRemix , ngoma hiyo huenda ilifanyika miaka kadhaa iliyopita kutokana na kwamba Msanii #Radio hayupo duniani ametangulia mbele za haki.#RIPRADIO.

Related Articles

Check Also
Close
Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents