HabariTechnology

Donald Trump kuruhusiwa kutumia tena Facebook na Instagram

Donald Trump ataruhusiwa kurudi kwenye mitandao ya Facebook na Instagram, baada ya Meta kutangaza kumfungulia akaunti zake.

Akaunti zake zitafunguliwa “katika wiki zijazo”, kampuni kubwa ya mitandao ya kijamii ilisema.

Katika taarifa yake, Nick Clegg, rais wa masuala ya kimataifa wa Meta, alisema kuwa umma “unapaswa kusikia kile wanasiasa wao wanasema”.

Aliyekuwa rais wa Marekani alizuiwa kutumia Facebook na Instagram baada ya ghasia zilizotokea Capitol mnamo 2021.

Kampuni hiyo ilichukua hatua hiyo “baada ya Bw Trump kujisifu kuhusika katika ghasia katika ikulu ya Capitol”, Bw Clegg alisema.

“Maamuzi ya kumfungia mitandao yake ya kijamii yalikuwa ya ajabu kutokana na mazingira,” aliongeza.

Alisema uchunguzi umebaini kuwa akaunti za Bw Trump haziwakilishi tena hatari kubwa ya usalama wa umma.

Lakini kwa sababu ya “ukiukaji” wa zamani wa Bw Trump sasa atakabiliwa na adhabu kali kama makosa yakijirudia.

Republican wamekuwa wakishinikiza Bw Trump aruhusiwe kurejea kwenye mtandao wa Facebook anapojitayarisha kuwania urais tena mwaka ujao.

Bw Trump alichapisha kwenye kampuni yake ya mtandao wa kijamii, Truth Social, siku ya Jumatano, akisema kwamba Facebook “imepoteza Mabilioni” baada ya kumpiga marufuku “Rais wako kipenzi, mimi”.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents