Firmino amrejesha Philippe Coutinho, Liverpool ‘Nimekumisi sana kaka’
Nyota wa klabu ya Barcelona, Philippe Coutinho amejikuta akirejea Liverpool kwa mara nyingine tena huku safari hii ikiwa siyo kwaajili ya kuwatumikia majogoo hao wa Anfield.
Baada ya kuitumikia Liverpool kwa mafanikio makubwa ndani ya miaka mitano, Coutinho alijiunga na miamba hiyo ya Hispania mwezi Januari kwa dau la pauni milioni 145.
Usiku wa jana siku ya Jumatano, kiungo huyo mshambuliaji alirejea Merseyside kwaajili ya kumuunga mkono Mbrazili mwenzake Roberto Firmino ambaye alikuwa akisherehekea siku ya kuzaliwa kwa mkewe, Larissa Pereira.
Baadhi ya waliyohudhuria kwenye sherehe hiyo ‘all-white affair’ na kunaswa na video ni Firmino na Alberto Moreno ambao wameposti pia kupitia ukurasa wao wa kijamii wa Instagram.
Coutinho ameonekana akiwa mwenye furaha tele karibu na Firmino, Moreno pamoja na Mbrazili mwenzao Fabinho.
https://www.instagram.com/p/BrTBXw5AiR8/?utm_source=ig_embed
Kupitia Instagram stori, Moreno ameandika ”Nimekumisi sana kaka”, huku wakioneka kufurahi pamoja na Coutinho.
Kwenye sherehe hiyo ya kuzaliwa kwa Larissa Pereira kulikuwa pia na baadhi ya nyota wa klabu ya Liverpool wanaocheza sasa na hata wa zamani wakionekana wakifurahi kwa pamoja usiku huo.